Wadau mbalimbali wametembelea Banda la Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) . Kupitia maonesho hayo, GST imeendelea kuwaelimisha na kuwafahamisha juu ya masuala mbalimbali ikiwemo aina za madini na miamba inayopatikana katika maeneo mbalimbali ya nchi; huduma zitolewazo na GST; na njia za kisayansi zinazotumika katika utafutaji, uchimbaji na uchenjuaji Madini.
