Balozi wa kudumu katika Ofisi za Umoja wa Mataifa nchini Marekani Dkt. Sulemain Haji Suleiman amefanya kikao kazi na timu ya wataalam wa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) jijini Dodoma kwa lengo la kujifunza kuhusiana na fursa za uwekezaji katika sekta ya madini kwa upande wa madini mkakati kama vile Lithium , Nickel na Cobalt.

Balozi wa kudumu Tanzania katika ofisi za Umoja wa Mataifa nchini Marekani Dkt. Suleiman Haji Suleiman pichani akijadiliana jambo na timu ya wataalam wa jiosayansi kutoka katika Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) hawapo pichani katika kikao kazi alichofanya jijini Dodoma
Mwakilishi wa kampuni ya Heritage Group ya nchini Marekani kwa upande wa Tanzania akizungumza jambo wakati wa kikao kazi na timu ya wataalam kutoka GST.
Timu ya Wataalam kutoka GST ikifuatilia jambo kwa makini wakati Balozi Dkt,Haji Suleiman Haji akizungumza wakati wa kikao kazi kilichofanyika mkoani Dodoma.